17th October, 2016
Wanahabari Asha Mwilu na Rashid Iddi wa kampuni ya Standard Group walifika humu nchini jumapili usiku na kupokelewa kwa bashasha kufuatia ushindi wao wa tuzo za uanahabari bora zaidi bara la Afrika za CNN. Wawili hao waliwapiku washindani wengine na thelethini na nane kwenye hafla iliyofanyika afrika kusini wakijitwalia taji la wanahabari bora kufuatia taarifa yao ya upekuzi kuhusu shughuli za kigaidi katika mpaka wa Kenya na Somalia Terror Crossing. Dominic Omondi wa gazeti la The Standard pia aliibuka mshindi kwenye kitengo cha biashara na uchumi almaarufu The Ecobank Economic and Business Award. Cheboite Kigen kutoka kampuni ya The Nation Media Group akijitwalia tuzo la mpiga mpicha la Mohammed Amin Photographic