.
17th October, 2016
Gavana wa kaunti ya Mandera kapteni Ali Roba amelaani vikali kitendo cha watu kadhaa kushambuliwa na kujeruhiwa kwenye makabiliano kati ya genge la watu waliokua wakipinga orodha ya majina ya wanasiasa wapya waliotangazwa kwenye mkutano wa wazee wa jamii ya Garre, sehemu ya Takaba, kaunti ya Mandera. waathiriwa 6 walipata majeraha ya kuvunjwa miguu na mikono na kuhamishwa hadi katika hospitali kuu ya mandera kupokea matibabu.