.
12th October, 2016
Mbunge wa Nyando Fred Outa ametoa wito kwa jaji mkuu mtarajiwa David Maraga kuahakikisha ameendelea na mabadiliko yaliyoanzishwa na mtangulizi wake Willy Mutunga katika idara ya mahakama. alisema hayo baada ya kukumbana na hali isiyotarajiwa pale alipotiwa rumande usiku kucha na mahakama ya Kisumu. Mbunge huyo amesema tofauti na matarajio yake, alikumbana na maji safi pamoja na vyoo katika rumande hiyo mbali na mapokezi mema kutoka kwa maafisa wa polisi.