25th September, 2016
Washindi na wale walioshamiri kwenye mashindano ya kriketi ya Qua-Drangular walitunukiwa hapo jana katika dhifa maalum iliyoandaliwa na shirikisho la kriketi nchini. Mashindano hayo yaliyoandaliwa nchini Kenya kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu yalishirikisha nchi nne zikiwemo Saudi Arabia, Qatar na Uganda. Kenya iliibuka na ushindi baada ya kuwalaza Saudi Arabia katika fainali. Miongoni mwa waliotunukiwa ni Nelson Odhiambo na Ifran Karim ambaye aliteuliwa mchezaji bora wa mashindano hayo.