19th September, 2016
Mahakama ya ICC imeamuru kuwa Kenya haikushirikiana nao katika kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta. kutokana na hilo Kenya imeshtakiwa mbele ya mataifa wanachama wa mkataba wa Roma. Majaji wa trial chamber 5b wanasema ni jukumu la mataifa wanachama kuamua hatua zitakazochukuliwa dhidi ya Kenya kwa kutoshirikiana na mahakama jinsi inavyohitajika kisheria. Tarehe 29 mwezi Novemba mwaka 2013 kiongozi wa mashtaka katika mahakama hiyo Fatou Bensouda alituma ombi la kutaka Kenya kuadhibiwa kwa kutoshirikiana na mahakama katika kutoa stakabadhi muhimu kwenye kesi dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta.Tarehe 3 Decemba 2014, majaji wa trial chamber 5(b) walitupa ombi hilo la kutaka Kenya kushtakiwa mbele ya mataifa wanachama wa mkataba wa Roma. Bensouda alikata rufaa tarehe 20 mwezi machi 2015, na tarehe 19 mwezi agosti mwaka 2015, mahakama ya rufaa ya ICC ikabatilisha uamuzi wake wa awali na kurejesha tena kesi hiyo mbele ya majaji husika.majaji wa trial chamber 5b wamesema kuwa tarehe 3 mwezi di