27th August, 2016
Zaidi ya ngamia 200 watashiriki katika mashindano ya kimataifa ya ngamia mjini Maralal. Ili kufanikisha mashindano hayo bodi ya utalii nchini KTB imefanya kliniki maalum ya kuwatibu na kuwatayarisha ngamia hao kwa mshindano hayo yanayofanyika katika kambi maalum ya ngamia ya Yare. Mashindano ya mwaka huu yakiwa yamewavutia watalii wengi zaidi kutoka maeneo mengine ulimwenguni kuliko mashindano ya miaka ya nyuma. KTB inanuia kutumia shilingi milioni kumi na nne kwa ufadhili wa mashindano hayo. Mashindano hayo ni ya kuonyesha tamaduni tofauti tofauti kutoka jamii zinazoishi katika kaunti ya Samburu kama vile Samburu, Borana, Turkana, Pokot na Rendille .