Viongozi wahudhuria kikao cha uchaguzi marekani
26th July, 2016
Kiongozi wa chama cha ANC Musalia Mudavadi na wa NARC Kenya Martha Karua wameelezea kujifunza mengi kwenye kongamano la chama cha democratic nchini marekani ambapo Hilary Clinton alipewa rasmi tiketi ya kugombea urais. Mudavadi na Karua wamekuwa miongoni mwa wakenya wachache waliohudhuria kongamano hilo la jana. Mudavadi amesema kwamba marekani ina uzoefu mkubwa kwenye masuala ya vyama vya siasa na jinsi ya kuvisimamia vyema kwa hivyo kutangamana na wanasiasa wa nchi hiyo kunaongeza maarifa yanayoweza kuboresha siasa za Kenya