David Kimaiyo azungumzia ufisadi katika viwanja vya ndege nchini
11th July, 2016
Aliyekuwa Mkuu wa Polisi David Kimaiyo hatimaye amezungumzia hatua ya kuondolewa kwenye wadhifa wa mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini. Kimaiyo amesema kuwa aliondolewa katika mamlaka hiyo kwa kukabili mienendo ya ufisadi uliokithiri. Rais Kenyatta alimwondoa Kimaiyo kwenye bodi hiyo baada ya kuhudumu kwa muda usiozidi miaka miwili. Kimaiyo kwa sasa anaendesha kilimo na ufugaji nyumbani,katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet.