Rais mstaafu Daniel Arap Moi amewahimiza wakenya kuendeleza masomo yao na kuinua uchumi wa Kenya
28th May, 2016
Rais mstaafu Daniel Arap Moi amewahimiza wakenya kuendeleza masomo yao na kuinua uchumi wa Kenya. Rais huyo mstaafu alisifu viwango wa elimu haswa katika shule za upili. Moi alitoa mfano wa shule ya upili ya kabarak ambapo asilimia 95 ya watahiniwa walifuzu kujiunga na vyuo vikuu katika mtihani wa kidato cha nne mwaka uliopita. Alikuwa akizungumza kwenye ibada ya maombi ya daktari Henry Kiptiony Kiplagat ambaye alifuzu na shahada la PHD. Daktari Kiptionyi amehudumu Kabarak kwa zaidi ya miaka ishirini na wakati mmoja aliwahi kuhudumu kama mwalimu mkuu wa shule za upili za Moi sacho na Moi Kabarak. Viongozi wengine walio hudhuria ni seneta wa Baringo Gideon Moi, waziri wa zamani wa michezo profesa Hellen Sambili na maafisa wakuu wa chuo kikuu cha Kabarak.