Wanasiasa wakashifu Serikali vikali kutokana na mauwaji ya Mwanabiashara, Jacob Juma
12th May, 2016
Serikali imekosolewa vikali wakati wa misa ya kumpa mkono wa buriani mfanyabiashara mashuhuri Jacob Juma katika kanisa la All Saints Cathedral jijini Nairobi. Viongozi wa upinzani na wanasiasa wa eneo la magharibi wameibua madai makali na kutoa wito kwa mkuu wa polisi, Bw. Boinnet, kukamilisha uchunguzi wakidai wauaji wa mfanyabiashara huyo wanajulikana. Francis Mtalaki na maelezo kamili.