Hofu ya kuzuka kwa maradhi ya Kipindupindu imetanda katika shule ya upili ya wavulana ya Narok
11th May, 2016
Hofu ya kuzuka maradhi ya Kipindupindu imetanda katika shule ya upili ya wavulana ya Narok baada ya zaidi ya wanafunzi 40 kufikishwa hospitalini wakiwa na dalili za kutapika na kuendesha . Baadhi ya wanafunzi walilalamikia kuumwa na tumbo. Hata hivyo mwalimu mkuu wa shule hiyo amefutilia mbali madai kuwa huenda wamekula chakula kichafu. Watabibu wangali wanachunguza ugonjwa huo. Wanafunzi 814 , walimu na wafanyikazi 200 wa shule hiyo wamepokea dawa za kuangamiza viini vya kipindupindu.Maafisa wa afya pia wanachunguza hali ya usafi wa maji yanayotumika shuleni humo.