Jengo laporomoka Nyali, Mombasa
9th May, 2016
Wiki 2 baada ya mkasa wa jengo kubomoka katika mtaa wa Huruma hapa Nairobi, sehemu ya jengo moja mjini Mombasa imeporomoka. Jengo hilo lenye duka la jumla la Naivas na maduka mengine ya rejereja katika mtaa wa Nyali lilibomoke sehemu ya vyoo usiku wa kuamkia leo. Kulingana na mamlaka ya kaunti ya Mombasa,hakuna aliyejeruhiwa kwenye mkasa huo.