Gavana Evans Kidero awapa wamiliki wa vyumba siku 90 kuhakikisha majengo yao yamekaguliwa
8th May, 2016
Gavana wa Nairobi Daktari Evans Kidero ametoa makataa ya siku tisini kwa wamiliki wa vyumba jijini nairobi kuhakikisha kwamba majengo yao yamekaguliwa la sivyo yabomolewe. Makataa hayo yanatolewa kufuatia kuporomoka kwa jengo la makazi katika mtaa wa huruma na kuwaua watu zaidi ya hamsini ijumaa iliyopita.gavana kidero ambaye alikuwa akizungumza katika kanisa la all saints cathedral baada ya hafla maalum kwa askofu eliud wabukala anayestaafu baada ya kuhudumu kwa miaka 7, amesema kwamba changamoto katika kubomoa majengo hayo ni pale wamiliki wanapoelekea mahakamani na kupinga ubomozi.