Idadi ya walioaga dunia katika mkasa wa Huruma yafikia 51
8th May, 2016
Idadi ya walioaga dunia kufuatia mkasa wa huruma imefikia 51, hii ni baada ya miili miwili zaidi kupatikana usiku wa kuamukia leo. Aidha wale wasiojulikana waliko wameripotiwa kuwa 28 huku shughuli za uokozi zikielekezwa katika mto nairobi katika muda wa mwisho mwisho wa shughuli hiyo. Shughuli ya uokozi imechukua zaidi ya siku nane sasa huku wanaotakiwa kuhama kutoka nyumba zinazopakana na jumba la mkasa wakilalamikia mpangilio duni.