Miili minne yapatikana katika maafuriko wa jumba la Huruma
7th May, 2016
Miili mingine mitatu imepatikana leo eneo la mkasa wa Huruma na kufikisha idadi ya waliofariki hadi 48 huku ubomozi wa makazi hatari ukiendelea. Kufikia sasa, idadi ya watu waliookolewa ni 140 huku ya wasiojulikana wakiwa 55. Aidha, mifugo zaid wanaendelea kupatikana wakiwemo kuku, bata mzinga na paka kufikia saa kumi za jioni. Nao wakazi wa majumba yaliyokaribiana na eneo la mkasa wakiendelea kuhama. Shughuli ya kubomoa majumba manane mtaani pia inaendelea.