Tume ya IEBC imesema hawatabanduka uongozini kutokana na vitisho vya WanaCORD
5th May, 2016
Tume ya uchaguzi IEBC imekariri kuwa makamishna wake hawatabanduka uongozini kutokana na vitisho vya WanaCORD. Kwenye kikao cha wanahabari mwenyekiti wa tume hiyo Isaack Hassan amesema makamishna wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kama ilivyo chini ya katiba. Tume hiyo sasa imewataka WanaCORD kukoma kuwasuta na kumtaka kinara wa muungano huo Raila Odinga kutoa ushahidi kuthibitisha madai kwamba tume ina njama ya kuhusika kwenye wizi wa kura . Francis Mtalaki anaarifu