Wafanyikazi na viongozi Bungoma wataka mkataba wa Pan-Paper kuwekwa wazi
4th May, 2016
Licha ya tangazo la serikali wiki jana la kufunguliwa tena kwa kiwanda kilichofilisika cha Pan-Paper mjini Webuye kaunti ya Bungoma, baadhi ya wafanyikazi na viongozi wa eneo hilo wameelezea wasiwasi wao juu ya uhalisia kamili wa mkataba ulioafikiwa kukiuza kiwanda hicho kwa muekezaji wa kibinafsi, huku wakiitisha mkataba huo kuwekwa wazi.