Peter Munya awaongoza magavana wenzake kumfariji rais mustaafu Mwai Kibaki
3rd May, 2016
Mwenyekiti wa baraza la magavana Peter Munya awaongoza wenzake kumfariji rais mustaafu Mwai Kibaki kutokana na kifo cha mkewe mama Lucy Kibaki . Wakati huo huo serikali imetoa ratiba ya maziko ya Mama Lucy Kibaki.. Ibada ya wafu itafanyika katika kanisa la Consolata Shrine. Mipango hiyo imetangazwa na katibu katika wizara ya mambo ya nje Karanja Kibicho.