Miujiza: Mtoto wa miezi saba aokolewa akiwa hai kutoka kwa vifusi vya jumba lililoporomoka Huruma
3rd May, 2016
Tunaanza kwa habari njema kutoka sehemu ya tukio la maporomoko ya nyumba mtaani Huruma ambapo mtoto wa kike wa miezi saba aliokolewa akiwa hai saa kumi alfajiri ya leo. Kulingana na waokozi wa shirika la msalaba mwekundu, mtoto huyo amekuwa kwenye vifusi vya jumba hilo kwa siku nne. Aidha mwili wa mwanamke mmoja ulipatikana kwenye chumba alichokuwa mtoto huyo.