Msasa wa vyeti vya elimu ya mbunge wa Kabete Ferdinand Waititu
2nd May, 2016
Tetesi na cheche za maneno baina ya gavana wa Kiambu William Kabogo na mbunge wa Kabete Ferdinand Waititu kuhusiana na elimu ya mbunge huyo zinazidi kugonga vichwa vya habari huku Kabogo akisema kuwa Ferdinand Waititu alitumia vyeti ghushi vya shule kuwania nafasi ya Ugavana na kutumia jina la Clifford Ndung’u Waititu anayeaminika kuwa ndugu yake. Mwanahabari wetu mpekuzi Mohamed Ali amekuwa akifuatilia matukio haya na kutuandalia taarifa ifuatayo