Rais Kenyatta akashifu vikali uwindaji haramu katika mipaka ya Kenya
30th April, 2016
Wawindaji haramu wameonywa dhidi ya kuendelea kushiriki biashara haramu kuuza pembe za Ndovu na vifaru. Katika hafla ya kuchoma pembe za ndovu iliyoandaliwa katika makao makuu ya shirika la uhifadhi wa wanyama pori nchini kenya, viongozi mbalimbali walisema tabia hiyo inatakiwa kukomeshwa mara moja. Rais wa garbon ali bongo alikuwa miongoni mwa wasemaji waliokemea kwa dhati hulka ya uwindaji haramu. Mbali na mwenyeji wao rais uhuru kenyatta, ujumbe kutoka marekani na ufaransa ulitoa msimamo mkali dhidi ya wawindaji haramu.