Jopo la Tunoi laandika ukurasa mpya
27th April, 2016
Jopo la kumchunguza Jaji wa mahakama ya juu Philip Tunoi limeandika ukurasa mpya wa kufumbua ukweli kwenye sakata ya mlungula kwa kufika katika stesheni ya mafuta inayodaiwa kuwa ndipo hongo hiyo ilipopokelewa. Mpuliza kipenga Geofreey Kiplagat alitoa maelezo ya mambo yalivyokuwa siku hiyo na kisha jopo likarejea jumba la mahojiano. Francis Mtalaki na maelezo kamili.