Mswada wa jinsia wahairishwa bungeni
27th April, 2016
Spika wa Bunge la Taifa Justin Muturi amelazimika kuahirisha shughuli ya kupitisha mswada wa usawa wa jinsia baada ya Wabunge kukosa kufikisha idadi inayohitajika ili kujadili mswada huo. Shughuli hiyo imeahirishwa hadi alhamisi wiki ijayo. Baadhi ya Wabunge, akiwemo mwakilishi wa kike wa Kaunti ya Nyeri Priscilla Nyokabi wametoa wito wa kuahirisha shughuli hiyo kutoa nafasi ya mashauri zaidi kati ya wabunge ili mswada huo upitishwe kuwa sheria. Wabunge 195 waliunga mkono mswada huo kwa kuupigia kura huku 28 wakiupinga, hata hivyo idadi hiyo si ya kisheria kwa mujibu wa kanuni za bunge ndio maana imebidi kikao kuandaliwa tena hivi ndivyo mambo yalivyokuwa.