Chase bank yafunguliwa
27th April, 2016
Wateja wa Chase Bank mapema leo wamefurika katika matawi ya benki hiyo kuthibitishwa iwapo huduma zimerejeshwa. Benki ya Chase imewekwa chini ya mrasimu wiki tatu zilizopita. Baadhi ya wateja walionekana kuwa na matumaini kuwa kila kitu ki shwari sasa huku baadhi yao wakieleza kuwa mara tu benki itakapotatua matatizo yake bila shaka itakuwa benki ya kuaminika. Benki ya Chase sasa inasimamiwa na KCB. Meneja msimamizi wa benki hiyo kwa sasa Paul Russo ameahidi kuwa wako ngangari kuhakikisha kuwa wateja wake wanahudumiwa ifaavyo. Wateja waliopata huduma za benki hiyo kupitia mtandao waliruhusiwa kutoa hadi shilingi milioni moja pekee, kiwango kilichotajwa na benki kuu ya kenya wiki jana