Biwi la simanzi latanda katika kaunti ya Nyeri alikozaliwa marehemu Lucy Muthoni Kibaki
26th April, 2016
Katika maeneo ya Mukurweini alikozaliwa marehemu Lucy Muthoni Kibaki na Othaya , alikoishi na mumewe rais mstaafu, biwi la simanzi lilitanda kwa kumpoteza mwanamke waliyemtambua kama mama. Wengi walimsifu kwa jitihada zake za kuanzisha miradi ya ufanisi ambayo imewasaidia watu hasa wale waliozongwa na umaskini.