Serikali ya Jubilee inaitaka mahakama ya ICC kuwasilisha faili za wanaodaiwa kuwaingilia mashahidi
21st April, 2016
Sasa serikali ya Jubilee inaitaka mahakama ya ICC kuwasilisha faili za wanaodaiwa kuwaingilia mashahidi ikisema kuwa itaunda mahakama hivi karibuni kushughulikia madai hayo yanayolimbikiziwa watuhumiwa Walter Barasa, Paul Gicheru na Phillip Bett. Kulingana na mwanasheria mkuu nchini profesa Githu Muigai, Kenya imeshirikiana na baadhi ya mataifa chini ya mwavuli wa umoja mataifa ya Afrika kwenye mazungumzo ya iwapo bara Afrika litajiondoa katika mahakama ya ICC au la.mwanahabari Francis Mtalaki na melezo kamili.