Wakaazi wa Kajiado waghadhabishwa na hatua ya wawakilishi wadi kusususia hotuba ya gavana Nkedianye
18th April, 2016
Wakaazi wa kaunti ya Kajiado wameghadhabishwa na wawakilishi wadi kwa hatua yao ya kusususia hotuba ya gavana David Nkedianye siku chache zilizopita. Baadhi yao wanasema hatua hiyo inaashiria wawakilishi wadi hao wamesahau majukumu yao. Sasa wametishia kuliondoa bunge lote la kaunti kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2017 iwapo hawataheshimu taasisi ya gavana.