Wavuvi wanaoishi maeneo yanayo nuiwa kujengwa mradi wa SGR walalamikia mpango wa fidia
18th April, 2016
Wavuvi wapatao 1700 wanaoishi katika maeneo yanayo nuiwa kujengwa mradi wa Standard Gauge Railway na kivukio cha Dongokundu sasa wamejitokeza kuulalamikia mpango wa fidia. Wavuvi hao wamekashifu mkondo uliochukuliwa na serikali kupunguza fedha za kuwafidia kutoka bilioni 2.1 hadi milioni 980.