Wasichana 300 waliokwepa kupashwa tohara wahitimu katika mafunzo mbadala
16th April, 2016
Hali ya furaha na shamrashamra ilidhihirika mjini Maralal katika Kaunti ya Samburu baada ya wasichana 300 waliokwepa kupashwa tohara kuhitimu baada ya mafunzo mbadala . Wasichana hao walifunzwa kuhusu umuhimu wa elimu na ubaya wa upashaji tohara . Sherehe hiyo iliyoandaliwa na viongozi wa eneo hilo wakishirikiana na mashirika yanayopinga tohara ya wasichjana ilibarikiwa na wazee wa eneo hilo walioapa kupinga tohara kwa mtoto wa kike.