Mwanahabari wa shirika la Standard David Odongo alikamatwa kwa kuandika taarifa Kimani Rugendo
16th April, 2016
Mwanahabari wa shirika la Standard anayeandikia gazeti la Nairobian ameachiliwa baada ya kulala korokoroni. Maafisa wa polisi walikuwa wamemkamata David Odongo hapo jana kwa kuandika taarifa kuhusu bilionea kimani Rugendo. Polisi walimzuilia odongo katika kituo cha polisi cha embakasi ila hawakusema kosa alilokuwa amefanya.