Kinara wa chama cha NARC Kenya Martha Karua awasuta viongozi wa Jubilee kuhusu mkutano wa maombi
15th April, 2016
Kinara wa chama cha NARC Kenya Martha Karua amewasuta wakuu wa serikali kwa mpango wa kufanya maombi katika uwanja wa afraha katika kaunti ya nakuru kama njia ya kusherehekea ushindi wa naibu wa rais William Ruto na mwanahabari joshua sang katika mahakama ya icc. Karua amesema kuwa wakati viongozi hawa wakisherehekea, waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007 wangali hawajafidiwa na kusalia katika tabu kutoka na ghasia hizo.