Aliyekuwa afisa mkuu mtendaji wa benki ya National Munir Ahmed ahojiwa na CID
11th April, 2016
Huku wateja wa benki iliyowekwa chini ya mrasimu wakisubiri suluhu ya kuwarejeshea pesa zao, benki kuu imeanza leo kutoa ufadhili kwa benki zinazojipata kwenye matatizo ya kifedha bila kukusudia. Wakati huo huo aliyekuwa afisa mkuu mtendaji wa benki ya National Munir Ahmed na Mameneja wengine watatu wamehojiwa katika makao makuu ya idara ya upelelezi nchini hapa Nairobi.