Abiria wanusurika kifo baada ya ajali kutokea katika eneo la Kibarani, Mombasa
10th April, 2016
Watu kadhaa walinusurika kifo katika eneo la Kibarani Mombasa,baada ya lori lililokuwa likielekea mjini mombasa kupoteza mwelekeo na kugonga matatu iliyokuwa ikielekea Changamwe. Matatu hiyo ilibingiria mara kadhaa na kusababisha gari jingine kuingia bondeni. Waathiriwa walipelekwa katika hospitali kuu ya Coast General wengi wao wakiwa wamevunjika miguu na mikono.