Francis Atwoli ataka umoja wa jamii ya wanacord
8th April, 2016
Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi nchini Francis Atwoli amelaani vikali kisa cha mkutano wa Seneta Wa Bungoma Moses Wetangula kuvurugwa na kikundi fulani cha watu. Atwoli aliyezungumza akiwa Nambale katika Kaunti Ya Busia mapema leo, amesema kwamba kila kiongozi kutoka magharibi ya Kenya ana uhuru wa kutangaza azma yake kugombea urais kokote anakotaka.