Jaji mkuu Willy Mutunga atoa faili ya kesi ya Dedan Kimathi kwa chama cha Mau Mau
4th April, 2016
Jaji mkuu Dkt Willy Mutunga ametoa faili ya kesi ya Dedan Kimathi kwa chama cha Mau Mau, kwenye hafla maalum iliofanywa katika bustani ya freedom corner jijini nairobi. Katibu wa chama cha mau mau Gitu wa Kahengeri ameipokea faili hiyo yenye maelezo ya kesi iliyomkumba kiongozi wa mau mau Dedan Kimathi.