Msemaji wa serikali Eric Kiraithe awashtumu wanasiasa wanaotumia ghasia na vitisho
3rd April, 2016
Msemaji wa serikali Eric Kiraithe amewashtumu wanasiasa na makundi ya kisiasa kwa kutumia ghasia na vitisho kuwatia hofu wapinzani wao. Kiraithe amewakosoa vikali wanasiasa kufuatia ghasia zilizozuka jumamosi katika bustani ya muliro kaunti ya Kakamega wakati kiongozi wa chama cha Ford Kenya Moses Wetangula alipokuwa akizundua azma yake kuwania urais katika uchaguzi mkuu mwaka ujao. Watu wawili waliripotiwa kujeruhiwa pale wafuasi wa gavana wa kaunti hiyo wycliffe oparanya na seneta bonni khalwale walipokabiliana. Mtu mmoja anadaiwa kurusha kitoza machozi kwenye umati .