Maswali yaibuka ni kwa nini haswa Kenya inashumbuliwa katika eneo la Afrika
2nd April, 2016
Ni mwaka mmoja sasa tangu kenya ishuhudie shambulizi baya zaidi la ugaidi, lililotekelezwa katika Chuo Kikuu Cha Garissa. Shambulizi la alfajiri lililosababisha vifo vya wakenya 148, idadi kubwa ikiwa ni wanafunzi.
Mauaji ambay o yamezua maswali chungu nzima, mbona Kenya ndio yenye kushambuliwa katika eneo hili la afrika mashariki? Je, ni kwa sababu ya kupeleka majeshi yake kwenye muungano wa amisom?, hali ya kenya kuwa mshirika mkuu wa mataifa ya magharibi katika jamii ya kimataifa? Au ni ukosefu wa ajira na mafunzo ya itikadi kali kwa vijana?