Wakazi 1000 wa kijiji cha Maungu, Voi wailaumu KWS kutaka kuwafurusha katika ardhi yao
30th March, 2016
Zaidi ya wakazi 1000 wa kijiji cha Maungu kaunti ndogo ya Voi wanalilia haki ya ardhi yao wanayodai kuwa shirika la wanyama pori KWS, linataka kuwafurusha baada ya kuishi hapo zaidi ya miaka 25. Wakazi hao sasa wanaitaka serikali ya kaunti ya Taita Taveta na serikali kuu kuingilia kati na kutetea haki yao.