Wawakilishi wa wadi wanawake waandamana kupinga kutolewa afisini kwa meneja wa jiji la Kisumu
29th March, 2016
Wawakilishi wa wadi wanawake wameshirkiana na raia kuandamana jijini Kisumu kupinga kutolewa afisini kwa meneja wa jiji la Kisumu Dorris Ombara. Waandamanaji hao ambao walianza matembezi nje ya jiji na kupenyeza hadi katikati na kusababisha msongamano mkubwa wa magari katika barabara kuu ya Kisumu Kakamega walibeba mabango na kuimba nyimbo za kumkashfu gavana Jack Ranguma. Duru zinaarifu ktn kuwa chanzo cha mvutano huo ni kitita kikubwa cha hela ambacho afisi ya meneja wa jiji inapokea kila mwaka ikiwa ni zaidi shilingi milioni hamsini.