Watu wawili wafa kwenye ajali Kakamega
25th March, 2016
Watu wawili wamepoteza maisha yao huku wengine 15 wakiendelea kupokea matibabu baada ya gari aina ya nissan la kuwabeba abiria kugongana na basi la kampuni ya Eldoret express usiku wa kuamkia leo. Ajali hiyo inasemekana kusababishwa na dereva wa basi alipojaribu kuipita tuktuk na kusababisha ajali.