Waititu asisitiza alimaliza digrii yake India
25th March, 2016
Mbunge wa kabete Ferdinand Waititu anasema atawasilisha hati kiapo dhidi ya gavana wa kiambu William Kabogo, kuhusiana na hulka zake za kimaadili kutokana na hali kwamba amehusishwa na visa kadha vinavyozua shauku kuhusu maadili yake. Akizungumzia kuhusiana na taarifa ya ktn leo hapo jana, tulipoangazia tu kwa muhtasari hati kiapo iliyowasilihwa na gavana Kabogo mahakamani kuhusiana na uhalali wa stakabadhi zake za elimu, Waititu anaelezea kwamba yeye ana majina yanayokanganya kutokana na hali kuwa wazazi wake walitengana wakati mmoja na kumlazimu kubadilisha jina. Ameahidi kuwasilisha mahakamani zaidi ya watu 50 aliyosoma nao kuthibitisha akuwa yeye anamiliki shahada.