Prof George Magoha achaguliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya baraza la mtihani
24th March, 2016
Aliyekuwa naibu mhadhiri wa chuo kikuu cha Nairobi George Magoha ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya baraza la mtihani hapa nchi baada ya kibiru kinyanjui kutimuliwa kwa misingi ya kushindwa kumaliza udanganyifu katika mitihani ya kitaifa. Kinyanjui ametimuliwa pamoja na maafisa wengine 9 katika baraza hilo waliotakikana na waziri wa usalama wa ndani Joseph Nkaissery kujiwasilisha kwa polisi na kuandikisha taarifa au kukamatwa.