Mkuu wa upelelezi Ndegwa Muhoro akosoana na wakili Ahmednassir Abdullahi kuhusu madai ya ufisadi
21st March, 2016
Mkuu wa idara ya upelelezi nchini Ndegwa Muhoro amekashifu vikali madai yaliomhusisha kupokea hongo pamoja na yale madai yaliyotolewa katika barua ya wakili Ahmednassir Abdullahi kuhusu mradi wa tatu city ambao kwa sasa unaonekana kuibua hisia mseto licha ya kesi hiyo kuwa mahakamani. Akizungumza na wanahabari,muhoro amewashauri mawakili wake kuanzisha kesi iwapo hatopata kusikia kutoka kwa wakili abdullahi.