Mbunge wa Rongai, Nakuru ahimiza tume ya TSC kuwaajiri walimu zaidi
20th March, 2016
Mbunge wa eneo la Rongai kaunti ya Nakuru Raymond Moi ametoa changamoto kwa waziri wa elimu Fred Matiangi na tume ya TSC kuajiri walimu zaidi ili kuimarisha elimu katika eneo bunge hilo. Moi alikuwa akizungumza katika shule ya upili ya burgei wakati wa uzinduzi wa miradi ya elimu utakaogharimu shilingi milion 7.2 unaofadhiliwa na serikali ya japan. Balozi wa japan nchini tatsushi terada alishuhudia shughuli hiyo. Aidha moi alitoa hundi ya shilingi elfu mia moja sabini na tatu ili kuwasaidia wanafuzi kutoka familia zisizojiweza.