Viongozi wa KANU waapa kuwania nyadhifa nyingi za kisiasa katika uchaguzi ujao
20th March, 2016
Viongozi wa chama cha KANU wamesema watahakikisha kuwa wanagombea nyadhifa nyingi za kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao. Wakizungumza katika hafla ya kuchangisha pesa katika shule ya msingi ya salawa kaunti ya baringo, viongozi hao wakiongozwa na mwenyekiti wa kanu gideon moi wamesisitiza kwamba hawatafika mbele ya tume ya IEBC kutoa mwanga zaidi kuhusu madai yao kwamba tume hiyo ilishirikiana na serikali kufanya udanganyifu kwenye uchaguzi mdogo wa seneti kaunti ya Kericho.