Gavana Joho: Nyumba za kisasa zitawanufaisha wengi Mombasa
19th March, 2016
Gavana Wa Mombasa Ali Hassan Joho amesisitiza kuwa wakaazi wanaoishi katika nyumba zinazomilikiwa na manispaa ya Kaunti Ya Mombasa ni lazima waondoke ili nyumba hizo zibomolewe na kisha majumba ya kisasa kujengwa . Joho alisema madhumuni ya mpango huo ni kuwafaa wafanyikazi wa manispaa ya Mombasa.Joho alisema kuwa kwa sasa ni wa chache ambao wananufaika na nyumba hizo akisema kuwa mpango wa sasa ni kuongeza idadi ya nyumba zinazoambatana na matakwa ya wafanyikazi.