Msaada wa Japan kwa Kaunti ya Nairobi
17th March, 2016
Serikali ya japan imeipa serikali ya kaunti ya nairobi msaada wa magari manne ya kuzimamoto. Magari hayo yanatarajiwa kuwa ya msaada mkubwa jijini kwani wakazi wengi wanaishi maeneo ya mitaa ya mabanda, ambapo mikasa ya moto hutokea mara kwa mara. Jiji la nairobi lina magari sita ya kuzima moto lakini mara nyingi ukubwa wa jiji unazilemea. Magari hayo manne ya thamani ya shilingi milioni mia mbili za kenya yatawasili miezi michache ijayo huku jiji hili likiwa mwenyeji wa kongamano la tokyo kuhusu maendeleo afrika au tikad, mwezi agosti mwaka huu.