Mtu mmoja auawa na wanne kujeruhiwa katika mzozo wa shamba, Njoro kaunti ya Nakuru
14th March, 2016
Mtu mmoja amefariki huku wanne wakipata majeraha ya mishale baada ya makundi 2 kuzozana katika shamba lenye utata la Ngongori sehemu ya Njoro kaunti ya Nakuru. Kulingana na kaimu mkuu wa polisi sehemu ya Njoro Janet Wasike, ghasia hizo zilianza baada ya jamii ya Waogiek kumshambulia mmiliki wa shamba aliyekua akilima.