Duale akosa imani na tume ya IEBC baada ya uchaguzi mdogo wa Malindi
13th March, 2016
Tukiwa tungali kwenye masuala ya siasa na uchaguzi, mbunge wa Garissa mjini Aden Duale sasa anaitaka tume ya iebc kujiuzulu kwa kile anachokitaja kuwa usimamizi mbaya wa uchaguzi mdogo huko malindi. Duale ambaye pia ni kiongozi wa wengi katika Bunge la taifa, amedai kwamba IEBC ilishindwa kuthibiti visa vya utoaji rushwa kwenye uchaguzi huo ambapo chama cha ODM kilishinda. Alidai kwamba matukio ya huko malindi ni picha halisi ya namna ambavyo huenda mambo yakawa katika uchaguzi mkuu ujao