Afisa mmoja wa IEBC akamtwa Nyeri akihamisha wapiga kura
12th March, 2016
Polisi huko mweiga, katika kaunti ya Nyeri wanawazuilia watu 13 miongoni mwao mwakilishi wa wadi katika kaunti ya laikipia na afisa wa tume huru ya uchaguzi na mipaka kwa kuwahamisha wapiga kura hadi katika kaunti ya Laikipia. mshukiwa huyo alikamatwa na polisi baada ya kupashwa habari na wananchi waliolalamika kuwa washukiwa hao walikuwa wakiwahamisha wapiga kura kinyume cha sheria. Afisa mkuu wa polisi kieni magharibi John Kemboi aliyathibitisha na kusema washukiwa hao walipatikana nyumbani kwa bi mmoja kwa jina Mary Wanjiru ambapo walimpata afisa huyo wa iebc na daftari la wapiga kura na mashine ya BVR.